Bei ya Subaru Forester Tanzania


Magari ya Subaru yameendelea kupata umaarufu zaidi nchini Tanzania miaka ya hivi karibuni, ikionekana watu wengi zaidi hasa vijana wakipendelea kuyaagiza. Hii inathibitishwa kwa kushika nafasi ya pili na ya sita katika magari maarufu yanayoagizwa kupitia kampuni za Beforward na Sbtjapan ikizipita Toyota Rumion, Harrier, Spacio na Nissan Juke.

Hapo zamani magari aina ya Subaru yalikua adimu kupatikana Tanzania, watu wengi waliyaogopa kutokana na ukosefu wa 'spare parts' vilevile magari haya yalihusishwa na magari ya mbio (racing cars) hivyo watu waliamini kuwa yanakula mafuta sana. Kwa mkoa wa Arusha hali ilikua tofauti kwani ukilinganisha na mikoa mingine Subaru ilikua maarufu kwa miaka mingi sana huko, hii ilisababishwa na kuwepo jirani na nchi ya Kenya. Kenya wamekua watumiaji wa Subaru kwa miaka mingi zaidi hadi kupeleka kuwa na official Subaru dealer nchini kwao, hii imesababisha upatikanaji wa 'spare' na 'service' kuwa rahisi kwa kipindi kirefu ukilinganisha na Tanzania.

Hali kwa sasa imebadilika,ingawa soko la Tanzania bado linashikwa na Toyota kwa asimilia 80%, kwa zaidi ya miaka tano au sita sasa uingizaji wa magari ya Subaru umeongezeka kwa kasi sana na kupelekea kushika soko kwa asimilia 3% baada ya Nissani yenye asilimia 4%. Ongezeko hili lilisababishwa na watu kugundua kuwa magari aina ya Subaru ni ya kawaida na yanauzwa kwa bei ya chini ukilinganisha na modeli sawa za Toyota. Kwa mfano mwaka 2016-2018 bei ya Subaru Forester 2008 uliweza kuipata kwa shilingi millioni 19 wakati Harrier 240G ilikua millioni 22 hadi 24 wakati huo. Kwa sasa bei zimepanda kutokana na wahitaji(demand) kuongezeka.

Fuji Heavy Garages ni kampuni ya Kitanzania ya urekebishaji wa magari ambayo kwa sasa imebobea zaidi kwenye magari aina ya Subaru, kwa msaada na ushauri wa bure kabla na baada ya kununua gari lako la Subaru unaweza kututafuta kwa kutumia mawasiliano haya.

Bei za Subaru Forester 2022

Forester ni mojawapo ya modeli za magari yanayotengenezwa na Subaru yenye muundo wa SUV, modeli hii ni maarufu zaidi ukilinganisha na nyingine kwa sababu ni kubwa na inafaa kwa matumizi ya familia. Bei hutegemeana na mwaka wa uzalishaji, hadi sasa kuna vizazi(generations) vitano vya uzalishaji wa gari hili kutokea mwaka 1997 lilipoanza kutengenezwa, hivi hujumuisha

Toleo la Kwaza (SF) 1997 - 2002

Toleo hili liliitambulisha Forester ulimwenguni, gari hili lilitengenezwa kwa kufuata muundo wa Impreza ambayo ni modeli nyingine ya Subaru yenye umbo dogo. Kwa sasa haya magari ni adimu na upatikanaji wake ni mgumu, hii inasababisha bei yake kuwa juu ingawa ni ya zamani.
Soko No. Usajili Bei Usafiri Ushuru (TRA) Clearance Jumla
Nje/Agiza NA Tsh 7,000,000 - 8,000,000 Tsh 3,172,000 Tsh 5,757,307.37 Tsh 1,500,000 Tsh 16,000,000 - 18,000,000
Ndani A** Tsh 7,000,000 - 8,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 7,000,000 - 8,000,000
B** Tsh 7,000,000 - 10,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 7,000,000 - 10,000,000
C** Tsh 7,500,000 - 10,500,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 7,500,000 - 10,500,000
D** Tsh 8,000,000 - 16,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 8,000,000 - 16,000,000

Toleo la Pili (SG) 2002

Toleo hili lilikua na mabadiliko kidogo ukilinganisha na la kwanza, toleo hili lilikua na uzito mdogo kwani lilitumia aluminium sehemu nyingi. Subaru Forester
Soko No. Usajili Bei Usafiri Ushuru (TRA) Clearance Jumla
Nje/Agiza NA Tsh 3,500,000 - 4,000,000 Tsh 3,172,000 Tsh 5,757,307.37 Tsh 1,500,000 Tsh 14,000,000 - 16,000,000
Ndani A** Tsh 7,000,000 - 8,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 7,000,000 - 8,000,000
B** Tsh 7,000,000 - 10,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 7,000,000 - 10,000,000
C** Tsh 7,500,000 - 10,500,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 7,500,000 - 10,500,000
D** Tsh 8,000,000 - 16,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 8,000,000 - 16,000,000

Toleo la Tatu (SH) 2008

Toleo hili ni maarufu kama 'Forester New Model' kwani modeli hii ilikuja tofauti na watangulizi wake kwa kuwa na umbo kubwa na kunyanyuka juu zaidi kwa urefu. Gari hili lina umbo zuri na bei yake haipo juu hii imepelekea watu wengi kuyaagiza na kufanya idadi yake kua nyingi ukilinganisha na vizazi vingine. Subaru Forester
Soko No. Usajili Bei Usafiri Ushuru (TRA) Clearance Jumla
Nje/Agiza NA Tsh 6,500,000 - 10,000,000 Tsh 3,172,000 Tsh 9,453,955.77 Tsh 1,500,000 Tsh 19,000,000 - 30,000,000
Ndani A** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
B** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
C** Tsh 11,500,000 - 15,500,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 11,500,000 - 15,500,000
D** Tsh 15,000,000 - 24,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 15,000,000 - 24,000,000

Toleo la Nne (SJ) 2012

Toleo hili lilizinduliwa mnamo mwaka 2012, vitu mbalimbali vilibadilika ikiwemo umbo la gari, pia mfumo wa gia ulibadilishwa badala ya 'automatic' uliwekwa mfumo mpya aina ya 'CVT'. Pia ilianza kutumia injini mpya ya Subaru aina ya FB20 badala ya EJ20. Subaru Forester
Soko No. Usajili Bei Usafiri Ushuru (TRA) Clearance Jumla
Nje/Agiza NA Tsh 11,500,000 - 30,000,000 Tsh 3,172,000 Tsh 12,217,416.66 Tsh 1,500,000 Tsh 28,000,000 - 46,000,000
Ndani A** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
B** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
C** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
D** Tsh 27,000,000 - 46,000,000 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 Tsh 27,000,000 - 46,000,000

Toleo la Tano (SK) 2018

Katika toleo hili Suabru iliendelea kutumia injini ya FB20 pamoja na ile ya FA20, vile vile waliongeza injine inayotumia umeme iitwayo e-Boxer. Subaru Forester
Soko No. Usajili Bei Usafiri Ushuru (TRA) Clearance Jumla
Nje/Agiza NA Tsh 46,000,000 - 65,000,000 Tsh 3,172,000 Tsh 27,630,741.69 Tsh 1,500,000 Tsh 77,000,000 - 96,000,000
Ndani A** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
B** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
C** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA
D** NA Tsh 0 Tsh 0 Tsh 0 NA